Quantcast
Channel: NYINGINE – ShaffihDauda
Viewing all 565 articles
Browse latest View live

Video-“Tulifikiri Simba wangetufunga 9 au 10”-kocha Gendarmerie

$
0
0

Baada Gendarmerie kupoteza mchezo wao kwa magoli 4-0 dhidi ya Simba, kocha mkuu wa timu hiyo Mvuyekure Issa amesema mawazo na fikra zao kabla ya mchezo huo ilikuwa huenda wakafungwa magoli 9 au 10 lakini kutokana na namna walivyopambana wameweza kupunguza idadi ya magoli.

Kwa kifupi kocha huyo anamaanisha kufungwa 4-0 na Simba kwa upande wao wamefanikiwa kwa sababu idadi ya magoli waliyotarajia kufungwa ni tofauti na ilivyokuwa baada ya mchezo.

“Timu yangu ina vijana wengi chipukizi na nimeitayarisha kwa muda mfupi kwa ajili ya mashindano haya. Kwetu (Djibouti) tupo nafasi ya tatu kwenye ligi lakini msimu uliopita ndio tulikuwa mabingwa wa ligi tukapata nafasi ya kuwajilisha nchi kwenye mashindano haya”-Mvuyekure Issa kocha mkuu Gendarmerie.

“Nilifikiri Simba itatufunga magoli 9 au 10 ndiyo tulikuwa tumezoea hivyo, lakini sasa hivi magoli yanazidi kupungua yamefika hadi manne, nadhani mwakani tutakuwa pazuri zaidi.”

“Tulikuja kucheza huku lengo letu kubwa ni kuzjia ili tusifungwe magoli mengi kwa sababu tulikuwa tunasikia wachezaji wa Simba ni machachari sana lakini sikuona kama tulivyokuwa tunatarajia.”

“Naenda nyumbani kujiandaa vizuri, nimeona makosa nitayarekebisha, tutajitahidi na sisi tupate ushindi nyumbani. Kila kitu kinawezekana kwenye mpira, siwezi kusema Simba watanifunga nyumbani. Titajitahi tupate ushindi ili tuwape faraja wadjibouti.”

“Magoli matatu yalitokana na makosa ya golikipa kwa sababu ndio amerejea kutoka kwenye majeraha amefanya mazoezi kwa siku chache ndiomaana hakuwa vizuri. Huyo ndio golikipa wa timu ya taifa pia.”

“Simba ni timu nzuri ina uwezo wa pesa inaweza kununua wachezaji wazuri na makocha wazuri pia.”


Ushindi finyu wa Yanga kimataifa, Shaffih Dauda ameona tatizo

$
0
0

Weekend iliyopita vilabu viwili vya Tanzania (Yanga na Simba) vilicheza mechi zao za kwanza za mashindano ya kimataifa msimu huu vikiwa kwenye uwanja wa nyumbani.

Jumamosi Yanga walicheza mechi ya Caf Champions League na St Louis kutoka Seychelles na kufanikiwa kupata ushindi wa goli 1-0, Jumapili ilikuwa ni zamu ya Simba ambao walishinda 4-0 dhidi ya Gendarmerie ya Djibouti kwenye mchezo wa Caf Confederation Cup.

Ushindi wa Yanga nyumbani unaonekana ni finyu kuliko matarajio ya watu wengi ukilinganisha na aina ya mpinzani waliekutana nae (St Louis).

Shaffih Dauda anadhani ushindi huo mwembamba walioupata Yanga dhidi ya St Louis unatokana na wachezaji kukosa motisha na morali.

“Yanga kama wamekosa motisha, wanacheza kama hawako tayari lakini ratiba inawataka kufanya hiyo. Moja ya maeneo ambayo Yanga wanahitaji kufanyia kazi kwa sasa ni kujenga morali ya wachezaji”-Shaffih Dauda, mchambuzi wa michezo.

“Inaweza kuwaathiri kimbinu na kiufundi kama saikolojia ya wachezaji haijakaa vizuri kuweza kutekeleza majukumu kutoka kwenye benchi la ufundi.”

Ilikuwa imezoeleka vilabu vya Tanzania kupata ushindi mkubwa dhidi ya vilabu vinavyotoka mataifa ya visiwani kama Comoros na Seychelles.

Yanga nawakumbusha ‘kushindwa kujiandaa ni kujiandaa kushindwa’

$
0
0

Na Baraka Mbolembole

MABINGWA wa soka Tanzania bara, Yanga SC watashuka tena dimbani Jumatano hii kuwavaa Majimaji FC katika mchezo wa raundi ya 18 ligi kuu Tanzania Bara. Yanga wapo nyuma kwa alama saba dhidi ya vinara-mahasimu wao Simba SC ambao watakuwa ugenini kucheza na Mwadui FC siku ya Alhamisi.

Ushindi ‘kiduchu’ katika mchezo wa raundi ya awali dhidi ya St. Louis Club kutoka Shelisheli katika ligi ya mabingwa Afrika haukuonekana kufurahiwa sana na wapenzi wa timu hiyo. Yanga walicheza kwa kiwango cha chini kwa mara nyingine huku baadhi ya wachezaji wakionekana kukosa morali.

Wanachopaswa kufanya

Kushindwa kufunga walau magoli mawili dhidi ya St. Lousi katika uwanja wa nyumbani upande wangu sitazami kama ni tatizo kwani katika misimu ya karibuni ya Caf mabingwa hao mara 27 wa kihistoria nchini wamekuwa na tabia ya kupata matokeo bora zaidi katika viwanja vya ugenini.

Msimu wa 2016 waliitoa APR ya Rwanda katika mchezo wa raundi ya kwanza baada ya kuifunga timu hiyo 1-0 ugenini. Matokeo ya nyumbani yalikuwa 1-1. Msimu uliopita pia tulishuhudia Yanga ikianza na ushindi wa 1-0 nyumbani dhidi ya wawakilishi kutoka Visiwa vya Comoro, Ngaya Club lakini waliweza kuichapa timu hiyo mabao 5-1 kwao na kusonga mbele, hivyo kwa aina ya timu ambayo wanacheza nayo sitazamii kuona wawakilishi wetu hao wanaondolewa katika michuano.

Yanga wapo katika michuano yote wanayopaswa kucheza msimu huu, wapo katika mbio za kutetea ubingwa wao wa ligi kuu, wapo 16 bora ya michuano ya FA Cup, pia wapo katika michuano ya Caf Champions league na kama watavuka raundi hii ya awali itamaanisha kuwa wataendelea kuwepo katika michuano ya Caf hadi mwezi wa nne kwa maana hata kama watatolewa katika raundi ya kwanza katika ligi ya mabingwa wataangukia katika michuano ya kombe la Shirikisho.

Wakati katika ligi ya mabingwa Afrika kukiwa na michezo miwili ya mtoano-nyumbani na ugenini, na ikiwa mshindi atashindwa kupatikana katika muda wa dakika 180 timu huingia katika upigaji wa mikwaju ya penati tano-tano na mshindi husonga mbele, katika FA Cup ni tofauti kidogo kwani timu hazipati nafasi ya kujiuliza baada ya dakika 90 za kwanza kumalizika.

Inapotokea kufungana kwa matokeo sheria ya mikwaju ya penati hutumika kusaka mshindi. Sidhani kama Yanga wamekuwa na maandilizi mazuri katika michezo ya mtoano. Katika michezo miwili ya FA walipata nafasi ya kucheza na timu za daraja la pili (Reha FC na Ihefu FC) sasa wanaenda kucheza na Majimaji FC katika mchezo ujao wa raundi ya 16 bora.

Dhidi ya Reha walifunga magoli mawili ndani ya dakika kumi za mwisho na kusonga mbele, walisubiri hadi dakika ya mwisho kabisa ya mchezo kusawazisha kwa kiki ya penati vs Ihefu jambo ambalo liliwapa nafasi ya kufika hatua ya kupigiana penati tano-tano.

Katika mikwaju hiyo Yanga ilipoteza penati ya tano ambayo Obrey Chirwa alikosa. Kama si ukosefu wa kujiamini Ihefu wangefuzu, lakini kipa Youthe Rostand aliweza kuzuia mikwaju mitatu na kuibeba timu yake hadi raundi ya 16.

Tangu kuanza kwa msimu huu Yanga imepoteza michezo miwili kwa njia ya penanati. Walipoteza mbele ya mahasimu wao Simba katika Ngao ya Jamii, pia walianguka vs URA ya Uganda katika nusu fainali ya michuano ya Mapinduzi.

Chirwa kwa upande wake ndiye mchezaji aliyepoteza mikwaju mingi ya penati kwa timu yake hadi sasa huku mara tatu akikosa ndani ya mwaka huu. Kwanini, kwa miaka mitatu sasa Yanga imekuwa ‘nyanya’ katika mikwaju ya penati? Chini ya Hans walipoteza mara kadhaa na sasa tayari naona wamejenga ‘tabia yao’ ya kutojiamini’ inapofika muda wa mikwaju ya penati.

Kitu kinachoshangaza zaidi si Chirwa tu anayekosa penati mara kwa mara, bali tatizo hilo lipo karibia kwa timu nzima jambo ambalo linaonyesha dhahiri kuwa timu hiyo haifanyii mazoezi ya kutosha eneo hilo. Kwa timu inayocheza michuano miwili ya mtoano ni makosa makubwa kutofanya mazoezi ya upigaji wa mikwaju ya penati na Yanga hawawezi kukwepa ukweli huu.

Hawajachelewa, wana wiki mbili za kujiandaa dhidi ya mchezo wa marejeano vs St. Louis pia wana wiki tatu za kujiandaa na mchezo wa FA dhidi ya Majimaji FC hivyo wanaweza kufanya mazoezi ili kujiimarisha zaidi kwa maana katika michezo hii ya mtoano ni rahisi game kufika katika hatua ya penati.

Yanga kama timu wameonekana kupoteza kujiamini kila inapofika wakati wa mikwaju ya penati na kama timu nyingine zingekuwa zinahimili mchezo wa kawaida dhidi yao na kulazimisha sare ndani ya dakika za kawaida za mchezo ni rahisi kwao kusonga mbele kama watatulia katika mikwaju ya penati.

Ili kurejesha kujiamini kwao katika upigaji wa mikwaju ya penati ni lazima wakubali kufanya sana mazoezi na kitendo cha kushindwa kufanya hivyo kitawaondoa katika michuano siku za mbeleni hata mbele ya wapinzani dhaifu.

Wanaweza kuiondoa St. Louis kwa vile timu hiyo ya Shelisheli imeonekana hainawezi kufunga na Yanga wanaongoza tayari lakini dhidi ya Majimaji tena katika uwanja wa Majimaji, Songea mahala ambako wameshinda mara moja tu katika kipindi cha miaka ya karibuni hii inaweza kuwa tofauti.

Majimaji wanaweza kuzuia Yanga wasifunge, pia wamekuwa na tabia ya kufunga goli/magoli vs Yanga jambo ambalo linaweza kuwa tatizo kwa mabingwa hao wa Bara. Nahodha wa zamani wa Jamhuri ya Ireland na Manchester United, Roy Keane ana msemo wake fulani ‘kushindwa kujiandaa, ni kujiandaa kufungwa’ hivyo Yanga wafanyie kazi kwa kiwango kikubwa upigaji wao wa mikwaju ya penati, ili kujiandaa na changamoto hiyo itakapowafika kwani wapo katika michuano ambayo inawalazimu kuwa tayari na bora katika upigaji wa mikwaju ya penati.

TFF imetangaza kumfungia Juma Nyoso

$
0
0

Kamati ya nidhamu ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) imetangaza kumfungia  Juma Nyoso wa Kagera Sugar kwa kosa la kupiga shabiki baada ya mchezo kati ya timu yake dhidi ya Simba kwenye uwanja wa Kaitaba, Bukoba.

“Kamati ya nidhamu ya TFF ambayo pia ilijadili mambo mengine, ilijadili shauri ambalo lilifikishwa kwenye kamati hiyo ambalo lilimuhusu mchezaji wa Kagera Sugar Juma Nyoso kuhusiana na tukio lake ambalo lilitokea kwenye mchezo uliozikutanisha Kagera Sugar na Simba kwenye uwanja wa Kaitaba”-Clifford Ndimbo, afisa habari TFF.

“Juma Nyoso alituhumiwa kumpiga shabiki baada ya kumalika kwa mchezo kinyume na kanuni za ligi kuu zinazozungumzia mchezo wa kiungwana.”

“Kamati ilipitia ripoti ya kamishna wa mchezo ambayo imeeleza tukio la kupishana kwa Juma Nyoso na shabiki ambaye alikuwa amebeba vuvuzela na Juma Nyoso akaonekana kusimama na kuanza kumpiga shabiki yule kwa kutumia kiatu na baadaye akamuinamisha na kuanza kumpiga kwa kutumia goti.”

“Kamati ilimwita Nyoso kujitetea, kwa upande wake alikataa madai hayo ya kumpiga shabiki. Alisema alichofanya ilikuwa ni kumkunja tu shabiki huyo lakini hakumpiga.”

“Kamati imemtia hatiani Juma Nyoso kupitia kanuni za ligi kuu na katiba ya TFF lakini ilipokea taarifa za nyuma za Nyoso kwamba aliwahi kuadhibiwa kwa makosa ya utovu wa nidhamu. Kwa hiyo kamati imemfungia Nyoso mechi tano pamoja na faini ya shilingi 1,000,000 (milioni moja).”

Yanga imepigwa faini

$
0
0
Klabu za Lipuli na Yanga kila moja imepigwa faini ya Tsh. 500,000 (laki tano) kwa kutumia milango isiyo rasmi kuingia uwanjani, kitendo ambacho ni ukiukaji wa Kanuni ya 14(14) ya Ligi Kuu. Adhabu dhidi yao imetolewa kwa kuzingatia Kanuni ya 14(49) ya Ligi Kuu kuhusu Taratibu za Mchezo.
 
Pia klabu ya Yanga imepigwa faini ya Tsh. 500,000 (laki tano) kwa kutoingia vyumbani, hivyo kwenda kinyume na Kanuni ya 14(13) ya Ligi Kuu kuhusu Taratibu za Mchezo. Adhabu hiyo ni uzingativu wa Kanuni ya 14(49) ya Ligi Kuu kuhusu Taratibu za Mchezo.

Goms United yasimamisha mabingwa Ndondo Super Cup

$
0
0

Goms United imefanikiwa kufuzu fainali ya Ndondo Super Cup baada ya kuifunga Itezi 3-2 katika mchezo  huo uliochezwa uwaja wa Bandari, Temeke, Dar es Salaam.

Misosi ni washindi wa pili wa Ndondo Cup 2017 Dar ambapo mabingwa wa taji hilo walikuwa Misosi huku Itezi wakiwa ndio mabingwa wa Ndondo Cup 2017 Mbeya.

Nahodha wa Itezi Romario Albert ameeleza sababu iliyopelekea timu yao kupoteza mcheo huo.

“Mechi ilikuwa nzuri tuliweza kutawala mchezo kwa dakika zote 90 lakini Mungu hakupenda, tumeshindwa kupata matokeo kwenye mchezo wetu. Wanambeya wasikate tamaa waziti kutu-support tunaweza kupambana tukachukua nafasi ya mshindi wa tatu”- Romario Albert.

Paul John amesema waliruhusu magoli mawili kipindi cha kwanza kutokana na kuidhauu timj ya Goms

“Tuliwadharau Itezi kwa sababu tjlikuwa tunacheza mpira kwa kuwaskilizia ndio maana kipindi cha kwanza walifanikiwa wakatufunga 2-1. Tulivyoingi vyumba vya kubadilishi kocha akatupa mbinu mpya za kutumia tukaongoza juhudi ndio maana tumepata matokeo.”

“Wapenzi wote wa Goms wakae mkao wa kula safari haturudii makosa kwa sababu mara kwanz tulitereza lakini safari hii tupo vizuri.”

Viongozi Toto Africans wagawana magodoro ya timu

$
0
0

Baada ya Toto Africans ya Mwanza kushuka daraja kutoka ligi daraja la kwanza hadi ligi daraja la pili, baadhi ya viongozi wa klabu hiyo wameanza kuchukua vifaa ikiwemo magodoro.

Mwenyekiti wa mashindano Wambura Mtani amesema kuna viongozi waliosafiri na timu kwenda Dodoma na Dar wakiwa na baadhi ya vifaa, hawajavirejesha vitu hivyo baada ya timu kurejea Mwanza.

“Wapo baadhi ya watu wameanza kugawana mali za Toto, wamechukua magodoro, sasa ukianza kuchukua vitu wachezaji wanaobaki na watakaokuja kwa ajili ya ligi daraja la pili watatumia nini?”-Wambura Mtani, Mwenyekiti wa Kamati ya mashindano Toto Africa.

“Tena sio wanachama tu bali ni viongozi wenye dhamana ambao wanatakiwa kuwa na uchungu na Toto, kuichangia lakini wao ndio wanakuwa wa kwanza kuchukua vitu vya klabu.”

“Wapo viongozi ambao waliondoka na timu kwenda Dodoma na baadae Dar kucheza FA Cup, kuna baadhi ya vifaa walichukua kwa ajili ya kwenda navyo nasikia havijarudi kambini.

“Tumekubaliana ikifika Jumatano mchana vofaa havijarudi, tunakwenda polisi kwa sababu huu ni wizi kama wizi mwingine.”

“Toto ni taasisi inapaswa itoke hapo ilipo ipande hadi daraja la kwanza na baadae ligi kuu kama ilivyokuwa.”

“Bocco atasafiri hata kama hatocheza”-Simba

$
0
0

Nahodha wa Simba John Bocco anatarajia kusafiri na timu kwenda Djibouti kwa ajili ya mchezo wa marudiano wa Caf Champions League dhidi ya Gendarmerie ingawa hakuna uhakika kama mshambuliaji huyo atacheza katika mchezo huo.

Bocco aliumia kifundo cha mguu wa kushoto wakati wa mchezo wa ligi dhidi ya Mwadui uliochezwa Alhamisi Februari 17, 2018 kwenye uwanja wa Kambarage Shinyanga na kushindwa kuendelea na mchezo.

Mjumbe wa kamati ya utendaji Simba, Said Tully amesema Bocco atasafiri na timu lakini walimu wamepanga kumpumzisha katika mchezo huo wa kimataifa.

“Bahati nzuri John Bocco hali yake sio mbaya ingawa walimu wanatarajia kumpumzisha kwenye mechi yetu tunayoenda kucheza Djibouti lakini ataambana na timu kwa sababu yeye ni captain, pamoja na kucheza ana jukumu la kuhamasisha wenzake ili kuweza kupata ushindi na kuendelea katika raundi ijayo”-Said Tully ameiambia Radio One.

Kikosi cha Simba kinatarajia kusafiri Jumamosi Februari 18, 2018 kuelekea Djibouti na wanatarajia kucheza siku ya Jumanne Februari 20, 2018. Mchezo wa kwanza Simba ilishinda 4-0 dhidi ya Gendarmeie kwenye uwanja wa Taifa.


Mwambieni Chirwa hajafikia thamani iliyomleta Yanga, Niyonzima ni mfano kuhusu anachowaza

$
0
0

Na Baraka Mbolembole

OBREY Chirwa amefunga goli lake la 11 msimu huu katika ligi kuu Tanzania Bara (goli moja pungufu ya yale aliyofunga katika msimu wake wa kwanza akiichezea Yanga SC).

Raia huyu wa Zambia amekuwa na habari nyingi tofauti tangu aliposajiliwa kutoka FC Platinum ya Zimbabwe, Juni 2016. Chirwa alitajwa kama mchezaji mwenye thamani kubwa zaidi katika soka la Tanzania baada ya kusajiliwa kwa kiasi kinachosemekana milioni 200 za Kitanzania.

Kama hiyo ndiyo bei yake iliyomleta ‘Jangwani’ hapana shaka yoyote kuwa anaendelea kubaki mchezaji ghali zaidi nchini. Kama sivyo ni nani sasa?

Muda

Chirwa alichukua muda mrefu sana kueleweka kiuchezaji ndani ya kikosi cha Yanga. Ujio wake ulivuruga mahusiano ya kimpira kati ya washambuliaji nyota wa Yanga, Mrundi Amis Tambwe na Mzimbabwe Donald Ngoma ambao kwa pamoja waliifungia Yanga jumla ya magoli 38 katika ligi kuu msimu wao wa kwanza wakicheza-pacha-2015/16.

Wakati timu ikiwa katika maandalizi ya msimu mpya na michuano ya makundi Caf Confederation Cup huko Uturuki, Ngoma na Tambwe walifikia hatua ya kutaka kupigana kufuatia Mzimbabwe huyo kumkebehi Tambwe na kumwambia ‘mwisho wako wa kutamba umefika.’

Ngoma na Chirwa walicheza pamoja huko Zimbabwe hivyo ujio wa Mzambia huyo katika kikosi cha Yanga kwake ulikuwa ni zaidi ya sababu za kimpira-urafiki pia ukihusishwa. Ndani ya uwanja alipoanza kucheza tu akiwa na jezi ya Yanga, Chirwa hakuonyesha kiwango kizuri kama mshambuliaji aliyesajiliwa kwa ajili ya kufunga magoli.

Alionekana ni mchezaji mzuri katika kumiliki mpira, kushambulia akitokea pembeni huku akitengeneza nafasi na kupiga pasi za magoli kwa wenzake. Hii haikuwa kazi aliyoletwa kuifanya Yanga ndio maana hata upande wangu niliamini awali mchezaji huyo ni ‘hasara’ katika kikosi ambacho tayari kilikuwa na wachezesha timu wengi.

Siku zote ‘muda’ huamua, na ndicho kilichokuja kutokea. Majeraha ya Donald Ngoma yalipomuanza msimu uliopita, Chirwa akaanza kupata nafasi ya kucheza sambamba na Tambwe katika safu ya mashambulizi. Akaanza kufunga vs Toto Africans, akafunga tena mara mbili katika ushindi wa Yanga 6-2 Kagera Sugar FC katika uwanja wa Kaitaba.

Kufunga kwake magoli manne katika michezo miwili ya Kanda ya Ziwa kulianza ‘kumsafisha’-kutoka katika ‘garasa’ na kuumia kwa Tambwe kulimfanya Chirwa apewe nafasi zaidi ya kucheza kama mshambulizi ambaye timu inamtegemea kufunga magoli.

Ushirikiano wake na Saimon Msuva ambaye alikuja kutwaa tuzo binafsi ya ufungaji bora mwishoni mwa msimu uliisaidia mno Yanga kutetea ubingwa wake kwa mara ya tatu mfululizo.

Namna alivyokuwa akicheza kwa kujituma baada ya kuaminiwa kwa kweli kulinifanya nigeuze maneno yangu na mara baada ya kufunga goli pekee la juhudi binafsi vs Azam FC nilisema ‘huyu Chirwa ni shujaa wa Yanga msimu huu’ hadi sasa naamini kitendo cha Yanga ‘iliyokosa makali’ kuishinda Azam FC 1-0 Aprili mwaka jana ndiyo kiliipa taji.

Katika soka ili upate mataji unalazimika kushinda michezo yako kabla ya kutegemea kushindwa kwa timu nyingine na ndicho walichofanya Yanga msimu uliopita hata kama kuna timu ziliwasaidia kwa kuifunga Simba waliokuwa wakishindana nao.

Chirwa alimaliza msimu wake wa kwanza akiwa amefunga magoli 12 katika VPL, matano katika FA cup.

Amepandisha thamani yake, ila hajafikia milioni 200

Kufunga magoli 12 kwa msimu kwa mchezaji aliyesajiliwa kwa lengo la kuifungia timu magoli si ‘haba’ hasa ukizingatia mchezaji mwenyewe ndiyo kwanza alikuwa akicheza Tanzania kwa mara ya kwanza, lakini kwa aina ya kiwango chake hadi sasa ni wazi Yanga ilikosea kumsaini kwa thamani ile kubwa.

Ndiyo alisaidia mno kuipa ubingwa msimu uliopita lakini ndani ya kikosi chao mchezaji aliyepaswa kuwa na thamani kubwa ni Msuva. Si kwasababu alishinda tuzo ya ufungaji bora , hapana, ni kwa sababu alionyesha yuko tayari wakati wote kuibeba timu yake hata wakati ikiwa katika ‘anguko la kiuchumi.’

Chirwa ameendelea kuwa na maendeleo mazuri kimpira ndani ya Yanga lakini nje ya uwanja ni mchezaji ambaye anapaswa kujitazama pia na kujithaminisha kama kweli anastahili kuwa mchezaji ghali zaidi wa klabu na katika soka la Tanzania.

Ameshafunga ‘hat-trick’ mbili msimu huu (mchezaji pekee kufanya hivyo msimu huu katika VPL hadi sasa), magoli 11 katika mzunguko wa 18 wa ligi, pia akiwa ameshakosa michezo sita kutokana na kufungiwa (mitatu mwanzoni mwa msimu kutokana na makosa aliyofanya katika mchezo wa mwisho msimu uliopita vs Mbao, na mingine mitatu alifungiwa Desemba-Januari).

Pia kuna michezo kama miwili alikosa kutokana na majeraha. Ukitazama vizuri idadi ya michezo aliyocheza katika ligi na idadi yake ya magoli utagundua kuwa Chirwa ametengeneza wastani wa kufuga goli moja kila mechi.

Lakini je hii inatosha kumfanya mchezaji huyo asajiliwe tena Yanga kwa thamani ya zaidi ya ile aliyoingilia? Upande wangu, hapana lakini kuelekea miezi yake minne iliyosalia katika mkataba wa sasa anaweza kuwashawishi watu wakampatia anachotaka.

Ila akumbushwe

Hakuna mchezaji aliyetoka Yanga moja kwa moja na kwenda kupata mafanikio Simba zaidi ya Mohamed Banka ambaye pia alisajiliwa Simba kama mchezaji huru baada ya kumalizika kwa mkataba wake Yanga na kunyimwa mpya katikati ya mwaka 2008.

Haruna Niyonzima ni mfano tu ambao anaweza kuutazama, japo Mnyarwanda huyo hawezi kuondoka mioyoni mwa wanayanga lakini alishapoteza nafasi ya kuwa mfalme klabuni hapo japo alifanikiwa kwa misimu sita aliyokuwa hapo.

Chirwa anapaswa kucheza zaidi na kuisaidia Yanga wakati huu wakipambana na kikosi chenye majeruhi wengi kutetea nafasi zao za uwakilishi Caf mwaka ujao. Kama Yanga itashindwa kufuzu kwa michuano ya Caf msimu ujao ni wazi thamani za wachezaji zitashuka tofauti na kama ikitokea wakafuzu.

Huu ni wakati wa mchezaji huyo wa Zambia kujiuliza kama kweli amelipa walau nusu ya milioni 200 ambayo analazimishwa kumaliziwa hivi sasa? Hata kama Yanga haitampa sasa, pesa yake itamfikia kwa maana ipo katika makubaliano rasmi, ila kuendelea ‘kususa-susa’ kucheza wakati huu hakusaidii klabu wala yeye mwenyewe, na kitendo cha kuwaza kuhusu Simba hivi sasa ni dhaifu ambalo linaweza kumuangamiza.

Miezi minne iliyobaki katika mkataba wa Chirwa na Yanga inaweza kuwa na thamani kubwa klabuni na kwa mchezaji mwenyewe kama atatuliza akili yake wakati huu uongozi ukipambana kuakikisha matatizo ya wachezaji yanatatuliwa.

Chirwa anaweza kutengeneza ufalme na maisha ndani ya Yanga maana shida za klabu zetu hizi zinatafutiwa ufumbuzi kuelekea mifumo mipya ya kiuendeshaji. Mwambieni, Chira ukipata kilicho bora Yanga ni ngumu kukikuta Simba, Niyonzima ni mfano tu, uhalisia tunaufahamu.

Afanye kazi ya mwajiri wake wa sasa na kuachana na mawazo ya kule anapotaka kwenda. Ataenda muda ukifika.

Fainali Ndondo Cup 2017 yajirudia 2018

$
0
0

Ile fainali ya Ndondo Cup 2017 kati ya Misosi FC dhidi ya Goms United hatimaye inajirudia tena katika fainali ya Ndondo Super Cup 2018 baada ya Misosi FC kufuzu hatua hiyo kwa kuifunga 2-0 timu ya Mnadani kutoka Mwanza.

Manahodha wa timu zote mbili wamezungumzia matokeo baada ya mechi kumalizika.

“Nimeumizwa na matokeo ambayo tumepata, tumefungwa 2-0 matokeo si mazuri kwetu kwa sababu hakuna mtu anayependa kufungwa”-Meshack Bona, nahodha Mnadani FC.

“Hakuna walichotuzidi isipokuwa walitumia vizuri nafasi walizopata lakini sisi tulishindwa kutumia nafasi tulizopata.”

“Tunajipanga vizuri hatuwezi kukata tamaa kwa sababu tumepoteza mechi ya leo, tutarekebisha mapungufu yaliyopo na kuongeza juhudi ili tushinde mchezo wa kufafuta mshindi wa tatu.”

“Kipindi cha kwanza hatukucheza vizuri kwakuwa tuliwadharau wapinzani wetu lakini tulivyoenda mapumziko tukakubaliana hii ni mechi kama zilivyo nyingine na hakuna sehemu ya kurekebisha makosa”-Emanuel Memba, nahodha Misosi FC.

Michuano ya Ndondo Super Cup ilianza jana Jumamosi Februari 17, 2018 kwenye uwanja wa Bandari-Temeke mchezo ulioshuhudiwa Goms United ikiuuzu fainali ya michuano hiyo kufuatia kufanikiwa kuifunga Itezi  United 3-2.

Nina uhakika Simba watasonga mbele, Yanga wafanye kazi”-Shaffih Dauda

$
0
0

Vilabu vya Simba na Yanga vinatarajia kuiwakilisha Tanzania katika michuano ya Afrika leo na kesho michezo ambayo itaamua nafasi ya ya vilabu hivyo kusonga mbele kwenye mashindano.

Simba inashuka uwanjani mucheza mechi ya marudiano dhidi ya Gendarmaie ikiwa na kumbukumbu ya ushindi wa magoli 4-0 katika mchezo wa kwanza uliofanyika Dar es Salaam hivyo Simba inahitaji ushindi au sare yoyote ili waweze kusonga mbele.

Yanga wao siku ya Jumatano watacheza mchezo wa marudiano dhidi St Louis ya Ushelisheli wakiwa wanafahamu ushindi au sare yoyote ndio itawafanya kuendelea na mashindano ya vilabu bingwa Afrika.

Mchambuzi wa masuala ya michezo Shaffih Dauda anaamini kwamba Simba wana asilimia nyingi za kuendelea na mashindano kutokana na matokeo waliyopata kwenye mchezo wao wa kwanza lakini anaamini Yanga wanatakiwa kufanya kazi ya ziada ili kusonga mbele.

“Mechi bado hazijamalizika, walicheza dakika 90 bado dakika 90 nyingine. Wote tulishuhudia mechi zilizopita namna ambavyo timu zetu zilicheza”-Shaffih Dauda.

“Yanga walipata matokeo, wamekwenda ugenini. Ushelisheli ni tofauti na ambavyo tuliwazoea zamani, wana timu nzuri na wana mipango, mechi ya nyumbani Yanga walishinda 1-0 kwa hiyo inabidi wafanye kazi kupata matokeo.”

“Simba wana akiba nzuri ya magoli waliyofunga kwenye mechi yao ya nyumbani, nina uhakika Simba watapeperusha vyema bendere ya Tanzania, Djibouti bado wana safari ndefu.”

Kocha wa msaidizi wa Simba Masoud Djuma amesema wachezaji wote wapo sawa kimchezo isipokuwa John Bocco ambaye aliumia kwenye mchezo wa ligi dhidi ya Mwadui pamoja na golikipa Aishi Manula aliyeumia kwenye mazoezi ya mwisho kabla ya mchezo huo.

“Tutapambana kama kawaida yetu tupate ushindi hapa au matokeo yoyote yatakayotufanya tuendelee mbele”-Masoud Djuma.

Mwanza imetoa mshindi wa tatu Ndondo Super Cup

$
0
0

Kabla ya kupigwa fainali ya Ndondo Super Cup 2018, ulichezwa mchezo wa kutafuta mshindi wa tatu wa mashindano hayo ambapo Mnadani FC wameibuka washindi baada ya kuifunga Itezi United kwa goli 1-0 kwenye uwanja wa Bandari.

Bao pekee katika mchezo huo limefungwa kipindi cha pili na Isac Neymar baada ya kuwazidi ujanja walinzi wa Itezi United.

Kocha wa Itezi United Faraja Richard amesema kujiamini kulikopitiliza ndio sababu iliopelekea timu yake kupoteza nafasi ya mshindi wa tatu wa Ndondo Super Cup.

“Nafikiri ni kujiamini kuliko pitiliza kwa wachezaji wangu walikuja wakiamini sisi ni timu nzuri na tutacheza vizuri, wameenda nje na vile ambavyo tulikuwa tumepanga kuvheza kitu ambacho kimetugharimu. Inaumiza kwa sababu hatukutegemea matokeo haya, tulipanga kucheza kwa namna nyingine lakini wamecheza tofauti kabisa”-Faraja Richard.

Kwa upande wa Manadani FC ‘Shehata’ amesema lengo lilikuwa ni kuwa mabingwa wa mashindano hayo lakini hata nafasi ya tatu kwao sio mbaya.

“Hata watazamaji waliotuona tumecheza mechi ya kwanza halafu wakaona tulivyocheza leo wamegundua tofauti kubwa.”

“Nashukuru kupata matokeo ya ushindi, kupoteza katika mchezo wa kwanza ilinikasirisha sana japo ndio matokeo ya mpira nilikubaliana nayo lakini nilijua mchezo wa leo nakuja kushinda”-Hassan Hosam ‘Shehata’

“Uwanja wa Kinesi ulikuwa unawasumbua wacheza, hofu, tension, lakini leo tumetulia na tumeshinda mchezo wetu.”

“Lengo langu lilikuwa kushinda ubingwa kwa sababu ilikuwa inawezekana lakini nashukuru kupata hata hii nafasi ya tatu sio mbaya.”

Febuari 21, 2018 ndio fainali ya Ndondo Super Cup, mechi ambayo itazikutanisha Goms United na Misosi FC ambazo zilicheza fainali ya Ndodo Cup Dar mwezi Agosti 2017 na kushuhudia Misosi wakitwaa ubingwa.

Kombe la Ndondo Super Cup limebaki Dar

$
0
0

Msosi FC wamefanikiwa kuwa mabingwa wa kwanza wa michuano ya Ndondo Super Cup 2018 baada ya kuendeleza ubabe dhidi ya Goms United kwa kuifunga 1-0 katika mchezo wa fainali uliochezwa kwenye uwanja wa Bandari.

Timu hizo zilikutana kwenye mchezo wa fainali ya Ndondo Cup 2017 ambapo Goms ilipoteza mchezo huo na kuiacha Misosi FC ikitwaa ubingwa kwa jiji la Dar es Salaam.

“Kwenye mchezo wa leo hakuna ambacho wachezaji wa misosi walituzidi ila wametumia ujanja wa kupita kwa beki wetu wa kushoto ambaye alipata majeraha na wao wakatumia fursa hiyo kupta goli”-Shabani Kazumba ‘Mourinho’, kohcha Goms United.

“Baada ya kugundua kwamba nilifanya kosa la kuchelewa kufanya mabadiliko kumtoa mchezaji aliyeumia, tayari dakika hazikuwa rafiki mwisho wa siku tumepoteza mchezo.”

Kocha wa Misosi FC ametamba kuwa, hata akiamshwa usiku acheze dhidi ya goms lazima atawakalisha kwa namna yoyote ile.

“Mara nyingi goms kwangu mimi huwa hawakohoi, mara nyingi huwa najipanga na timu yangu kama watu waliona mechi yetu iliyopita nilichezesha wachezaji wengi ambao hawafahamiki sana na wakatupa matokeo. Hata nikiamshwa usiku wa manane nicheze na Goms nampiga.”

Mashindano ya kombe la Ndondo Super Cup yalishirikisha timu nne za mikoa mitatu tofauti ambayo michuano Ndondo Cup 2017 ilichezwa. Itezi United (mabingwa wa Mbeya), Mnadani FC (mabingwa wa Mwanza) huku Dar ikitoa washiriki wawili Misosi FC mabingwa wa Dar na Goms United (washindi wa pili Ndondo Cup Dar)

Baada ya Yanga kufuzu kimataifa, “Sasa tunarudi kwenye ligi”-Kessy

$
0
0

Yanga imesonga mbele kwenye michuano ya vilabu bingwa Afrika licha ya kutoka sare ya kufungana 1-1 ugenini dhidi ya St Louis ya Seychelles ikiwa ni mchezo wa marudiano, vigogo hao wa VPL walishinda 1-0 katika mchezo wa kwanza uliochezwa uwanja wa taifa Dar hivyo Yanga wamefuzu kwa jumla ya magoli 2-1.

Ibrahim Ajib ndiye aliyeihakikishia Yanga kusonga mbele katika hatua inayofuata baada ya kuifungia timu yake goli dakika ya 45 kipindi cha kwanza lililoifanya Yanga iongoze, dakika ya 90+1 St Louis wakasawazisha na kufanya mchezo huo kumalizika kwa sare ya 1-1.

Mara baada ya mchezo huo kumalizika, mlinzi wa kulia wa yanga Hassan ramadhani ‘kessy’ amesema, walichokifuata Seychelles na sasa wanarudi kwa ajili ya kukomaa na VPL.

“Tulichokuwa tunakitaka tumekipata kwa hiyo wanayanga waendelee kutuunga mkono wasikate tamaa kwa mechi zijazo. Tumeshatoka hatua moja tumeenda nyingine, sasa tunarudi kwenye ligi”-Ramadhani Kessy, beki Yanga.

Yanga ambayo ndio bingwa mtetezi wa taji la VPL ipo nafasi ya pili kwenye msimamo wa ligi ikiwa na pointi 37 nyuma ya mnyama simba inayoongoza ligi kwa pointi zake 42. Yanga ikirejea nchini, mchezo wake unaofuata wa ligi ni dhidi ya Ndanda utaochezwa Nangwanda Sijaona, Mtwara.

Infantino ametaja sababu FIFA kuchagua kufanya mkutano Tanzania

$
0
0

Inawezekana ujio wa Rais wa FIFA gianni ifantino nchini pamoja na wajumbe mbalimbali wa shirikisho hilo la soka duniani umestua watu wengi ambao wanajiuliza kwa nini wamechagua kuja Tanzania halafu wanakosa majibu.

Infantino amesema wamekuja Tanzania kwa sababu shirikisho la mpira wa miguu duniani FIFA si la baadhi ya mabara wala baadhi ya nchi huko barani Ulaya bali ni shirikisho ambalo linaongoza nchi nyingi ambazo ni wanachama na kuja kwao nchini ni kuonesha namna ambacho wanajali kila nchi mwanachama.

Amesisitiza pia wamegundua mambo mengi baada ya mkutano wao ikiwa ni pamoja na namna ambavyo mkutano wao umefanikiwa, kuzidisha uhusiano kati ya FIFA na TFF na wanachama wengine wa FIFA.

“Kwa upande wangu kama Rais ni kuishi ambacho tunakisema kwamba FIFA ni shirikisho la mpira wa miguu duniani, hatuwezi kuendesha FIFA duniani kote wakati tunajifungia sehemu moja ni lazima tutoke kwenda kwa wadau wetu ambao ni vyama wanachama ambapo Tanzania ni miongoni mwao na kwa sababu hiyo ndiyo maana tupo hapa.”

“Kongamano lililofanyika hapa ni muhimu kwa sababu tumekutana na wawakilishi kutoka mabara mbalimbali (Asia, America ya Kati na Kaskazini, Caribean na Afrika) kwa ajili ya kujadili kuhusu maendeleo ya soka duniani ikiwemo mashindano ya soka la vijana na wanawake ambayo kwa kiasi kikubwa yamesahaulika.”

“Ni muhimu kuja huku kwa sababu ni miongoni mwa maeneo ambayo yalisahaulika na fifa, tumeamua kuja Tanzania hususan Dar es Salaam angalau kwa siku moja na kufanya shughuli rasmi ya kiofisi.”


Waziri Mkuu Majaliwa Kassim aunga mkono FIFA mapambano ya rushwa

$
0
0

Rais wa FIFA Gianni Infantino akiwa Tanzania kwa ajili ya kongamano maalumu la kutathmini maendeleo ya mpira wa miguu (The Executive Football Summit) alipata fursa ya kukutana na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Majaliwa Kassim.

Mh. Majaliwa ameupongeza uongozi wa FIFA kwa namna unavyosaidia maendeleo ya soka duniani.

“Tanzania inakupongeza sana kwa jitihada zinazolenga kuendeleza mpira wa miguu duniani kwa kutumia rasilimali zilizopo kwa malengo ya kuendeleza mpira.”

“FIFA ikiwa ni kitovu cha mapambano dhidi ya rushwa, na sisi Tanzania tunaunga mkono kwa kuhakikisha kwamba sekta zote za michezo zinatumia vizuri rasilimali zilizopo kwa ajili ya kuendeleza michezo lakini pia tunasimamia vizuri matumizi sahihi ya madaraka katika sekta za michezo ili kuleta maendeleo ya mpira wa miguu Tanzania.”

“Napenda kutamka kuwa tunaunga mkono jitihada hizi za FIFA CAF kwa mikono yetu miwili, ili kupata mafanikio makubwa katika mpira wa miguu hii ikiwa ni pamoja na kupata viongozi wenye muono wa mbali katika mpira wa miguu na mpango wa kuendeleza mpira wa miguu duniani kote.”

Ngumu kumeza iliyogusa, wachezaji, mawakala, usajili

$
0
0

Wakala wa mwanamichezo anatambulika kisheria kama mwakilishi wa kocha, mchezaji, kwenye mikataba ya michezo baina ya mchezaji na timu au  mwanamichezo na taasisi nyingine akisimamia haki za msingi pamoja na faida za mwakilishi wake kibiashara.

Wakala kwenye michezo ni rafiki wa mchezaji, mshauri, mbunifu wa masuala ya kimaendeleo kwa wanamichezo, msimamizi wa masuala ya kibiashara na wakati mwingine anaweza kuwa msimamizi wa haki.

Kabla ya miaka ya 1990, wachezaji wengi wa mpira wa miguu walikuwa hawatumii mawakala, wachache kati yao waliwatumia zaidi baba zao kama wawakilishi. Kutokana na wazazi wengi kutokuwa na uelewa wa masuala ya biashara ya mpira wa miguu, wachezaji wengi waliibiwa haki zao na wengine walilipwa ujira mdogo kuliko kilichotakiwa kwenye mikataba yao na vilabu.

Mpaka mwaka 1995 Sweden ilikuwa na mawakala watatu tu wa mpira wa miguu lakini hadi kufikia mwaka 2002 walikuwa na mawakala 33, kwa mujibu wa Fifa mpaka sasa kuna mawakala 5187 wenye leseni dunia nzima mawakala hao Italy ikitoa mawakala 600. Mawakala hupokea fungu la asilimia 4 mpaka 10 kutokana na mikataba ya wachezaji na hupata asilimia 10 mpaka 20 kutoka kwa makampuni au taasisi zilizowekeza fedha kwa mchezaji.

Kutoka enzi zile wachezaji wanaitwa kusajiliwa pale kwenye mgahawa wa chakula cha dunia, kuchukua pesa bila kuhesabu, shuhuda za wachezaji wanaosajiliwa kwenye ligi ya Tanzania zinastaajabisha na kuacha maswali mengi kichwani. Mtu mmoja anasema, wacha waendelee kutapeliwa muda mwingine wanayataka wenyewe.

Kama asilimia 4-15 akichukua msimamizi na kwenda kichwa-kichwa kupigwa na watu wa kati si kunatofauti kubwa sana? Pamoja na mvuto mkubwa aliokuwa nao Ulimboka Mwakingwe mwanzoni mwa miaka ya 2000, alisajiliwa na klabu ya Simba kwa kupewa seti ya sofa pamoja na baiskeli ya gia, tafakari tu katika hali ya kawaida endapo angekuwa na wakala kama biashara hiyo ingewezekana.

Mtu mwingine anaibuka anasema, mpira wa Bongo una maumivu kwa watu wengi, mkataba wa Geoffrey Mwashiuya unamalizika miezi minne ijayo kwenye klabu ya Yanga, kwa kilichomkuta kwenye usajili wa kwanza aliokuwa anatoka Mbozi kuja Dar angekuwa na wakala nadhani ‘kikombe kile kingemuepuka’.

Nauliza kwani ilikuwaje mzee baba? Jamaa anasema, pamoja na Nsajigwa kumfuatilia Mwashiuya kwa zaidi ya miezi mitatu pia vilabu vingine vilikuwa vinamfuatilia, Mwashiuya alitumiwa nauli akaja Dar alipofika tu akapokelewa na akina Seif Mandinga na Bin Kleb.

Mtoto wa Kinyiha kutoka Mbozi, alizuzuka bwana alipopanda vogue kwa mara ya kwanza kitu kilichomvuruga mpaka anaulizwa tukulipe mshahara kiasi gani Mwashiuya akajibu, nilipeni laki tatu tu kwa mwezi, wawakilishi wa Yanga walishikwa na kigugumizi cha mshangao mmoja wao akasema, unasema? Mwashiuya akajibu, laki tatu tu kina Mandinga wakasema, usiwaze kijana tutakulipa laki tano kwa mwezi.

Mzee mwenzangu huwezi kuamini, kwenye usajili wa Mwashiuya waliofaidika kwenye ule usajili ni timu ya Kimondo kuliko hata mchezaji. Kimondo walipata milioni 36 kutokana na mapato yote ya mlangoni waliyoyachukua kwenye mechi dhidi ya Yanga ambayo ilichezwa Vuawa. Biashara ilikwenda namna hiyo kutokana na mchezaji kutokuwa na msimamizi yeyote sio wakala wala meneja kitu kinachopelekea haki zake zingine kama bonus na vitu vingine visijadiliwe kwenye pande mbalimbali za mkataba huo.

Mtu mmoja anasema, wachezaji lazima wakubali kuwa na wasimamizi vinginevyo watatendewa vitu vya ajabu, huwezi kuamini, kuna mchezaji mmoja wa timu kubwa tu hapa nchini alisajiliwa na ahadi aliyopewa ilikuwa ni kupelekwa hospitali kufanyiwa tohara.

Jamaa mmoja anaibuka anasema, unakumbuka hata bishara ya Ngasa kwenda Sudan ilikwama kutokana na mchezaji huyo kutokuwa na msimamizi, Ngasa angekuwa na msimamizi si dhani kama msimamizi wake angekubali mchezaji wake azime simu na kujifungia hotelini juma zima wakati fuko la pesa likiwa linamtafuta, lakini wapotoshaji walitumia nafasi ya kutokuwepo wakala kumpotosha Anko ambaye kipindi hicho hakutaka kusikia la mtu yeyote hata Chibabubabu.

Hata Buswita angekuwa na msimamizi anayejitambua kuliko Mtabora si dhani kama angeshauriwa asaini mara mbili kwenye vilabu vya Simba na Yanga kisha wajifiche kwenye utetezi wa kupitiwa na Shetani.

Rashidi Mandawa ameisafishia njia Yanga Botswana

$
0
0

Mshambuliaji wa kimataifa kutoka tanzania anaecheza soka kwenye klabu ya BDF XI Rashid Mandawa, jana Jumatatu Februari 26, 2018 amefunga hat-trick dhidi ya township rollers ambao ni wapinzani wa yanga kwenye mchezo unaofuata wa hatua ya kwanza ya michuano ya vilabu bingwa Afrika (Caf Champions League).

Mandawa alifunga magoli hayo matatu kwenye mchezo wa ligi na kuisaidia timu yake kuibuka na ushindi wa magoli 3-1 ambao umeifanya ifikishe pointi 29 baada ya kucheza mechi 19 huku ikiwa kwenye nafasi ya sita ya msimamo wa ligi.

Hat-trick aliyofunga Mandawa dhidi ya Township Rollers imemfanya afikishe magoli 11 kwenye ligi kuu ya Botswana (BWPL) huku akiwa ametoa assists tano.

“Tangu nimejiunga na bdf nimefunga magoli nane na pasi tano za magoli (kabla ya mchezo dhidi ya township rollers)”-Mandawa.

Mandawa ameielezea kwa kifupi klabu ya Township Rollers ambayo kama wangekubabaliana huenda angekuwa anaitumikia kwa sababu kabla ya kujiunga na BDF alifanya majaribio kwenye klabu hiyo lakini hawakufikia makubaliano ili aweze kucheza kwenye timu hiyo.

“Kwa hapa Botswana Township Rollers ni timu kubwa kwa sababu ipo ki-professional zaidi, ukichagua timu bora inayoweza kushiriki ligi ya South Africa, Township rollers inaweza kuwa timu ya kwanza kwa sababu ina kila kitu, kwa Tanzania tunaweza kuifananisha na Azam kwa sababu Azam wana uwanja wao na kila kitu.”

“Ni timu kubwa yenye mashabiki wengi kama Yanga ilivyo tanzania. Township Rollers inashabikiwa karibu sehemu zote za Botswana na miongoni mwa timu inayopendwa sana. Yanga wanatakiwa kujua wanakutana na timu kubwa.”

“Safu yao ya ushambuliaji ndio hatari sana, wanaweza kuamua matokeo wakati wowote.”

Alivyopata mchongo kusukuma ngozi nje ya nchi

“Kuna mtu alinipa connection, sikuanzia hapa BDF XI nilianzia Township Rollers nikafanya trials pale lakini hatukukubaliana kwa hiyo nikahamia BDF  ambako nipo hadi sasa naendelea kufanya kazi

Ttofauti ya soka la Botswana na nyumbani

“Maisha ya Botswana kwa upande wa soka ni yaleyale na mara nyingi maisha ya mpira huwa hayabadiliki sana zaidi ni kupambana tu hakuna kinachobadilika.”

Samatta anampa machungu yasiyopimika

Maisha ya mpira ni mafupi sana, lakini ndoto zangu ni kufika mbali sana sio kucheza tanzania tu, nataka kufika mbali zaidi ili kuwa mfano bora zaidi kama anavyofanya mtanzania mwenzetu Mbwana Samatta kwa hiyo nataka kufika huko au zaidi ya alipo Samatta. Nasikia uchungu nikifikiria mwenzetu amefika vipi huko na sisi tunashindwa vipi.

Uendeshaji wa soka Botswana

Utofauti sio mkubwa sana mambo ni yaleyale lakini huku wenzetu wapo ki-professional zaidi kwenye level ambayo tunaweza kuifikia lakini tutachelewa. Ligi yao ni ngumu sana, ligi ya hapa na South Africa hazijapishana sana, kutoka botswana kwenda South Africa sio mbali sana na sio kazi kubwa kama unaonesha kiwango basi kwenda South Africa inkuwa kazi rahisi kuliko kutoka Tanzania.

Wasauzi kuhukumu Simba vs Al Masry

$
0
0

Shirikisho la mpira wa miguu Afrika (CAF) limewapanga waamuzi kutoka nchini Afrika Kusini kuchezesha mchezo wa Kombe la Shirikisho barani Afrika wakati Simba itakapocheza na Al Masry ya Misri Machi 7, 2018 uwanja wa Taifa saa 10:00 jioni.

Mwamuzi wa kati atakuwa Thando Helpus Ndzandzeka akisaidiwa na Zakhele Thusi Siwena mwamuzi msaidizi namba moja na Athenkosi Ndongeni mwamuzi msaidizi namba mbili wakati mwamuzi wa akiba atakuwa Christopher Harrison na kamishna wa mchezo huo Tuccu Guish Chrbremedhin kutoka Eritrea.

Mchezo wa marudiano utachezwa huko Port Said Machi 17, 2018 utachezeshwa na waamuzi kutoka Eritrea.

Mwamuzi wa kati atakuwa Yonas Zekarias Ghetre akisaidiwa na Angesom Ogbamarian mwamuzi msaidizi namba moja na Yohannes Tewelde Ghebreslase mwamuzi msaidizi namba mbili wakati mwamuzi wa akiba atakuwa Yemane Asfaha Gebremedhin na kamishna wa mechi hiyo atatoka Libya Gamal Salem Embaia.

Yanga vs Rollers kuamuliwa na warundi

$
0
0

Shirikisho la mpira wa miguu Africa (CAF) limewataja waamuzi kutoka Burundi kuwa ndio watachezesha mchezo wa ligi ya mabingwa barani Afrika kati ya Yanga dhidi ya Township Rollers FC ya Botswana utakaochezwa Machi 6, 2018 kwenye uwanja wa Taifa saa 10:30 jioni.

Mwamuzi wa kati atakuwa Pacifique Ndabihawenimana akisaidiwa na mwamuzi msaidizi namba moja Willy Habimana na mwamuzi msaidizi namba mbili Pascal Ndimunzigo wakati Kamishna wa mchezo huo anatoka Swaziland Mangaluso Jabulani Langwenya

Mechi ya marudiano itachezwa Machin 17, 2018 nchini Botswana na itachezeshwa na waamuzi kutoka Morocco.

Mwamuzi wa kati atakuwa Redouane Jiyed akisaidiwa na mwamuzi msaidizi namba moja Youssef Mabrouk na mwamuzi msaidizi namba mbili Hicham Ait Abou, mwamuzi wa akiba Samir Guezzaz na kamishna wa mchezo huo anatoka Afrika Kusini Gay Makoena.

Viewing all 565 articles
Browse latest View live


<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596347.js" async> </script>