Quantcast
Channel: NYINGINE – ShaffihDauda
Viewing all articles
Browse latest Browse all 565

#NDONDOCUP2016: UHURU SELEMANI ATUPA MBILI TEMEKE MARKET IKITINGA 16 BORA

$
0
0

IMG_0364

Sports Etra Ndondo Cup imeendelea tena leo kwenye viwanja viwili tofauti jijini Dar ikiwa ni hatua ya makundi.

Kwenye uwanja wa Chuo cha Utalii zamani uwanja wa Bandari, Temeke Market wameichapa Kinondoni FC mabao 2-1. Mabao yote ya Temeke Market yakiwekwa kambani na Uhuru Selemani wakati bao la Kinondoni FC likifungwa na Vicent Costa.

IMG_0363

Brian yeye ni nahodha wa timu ya Temeke Market ambaye hajasita kuisifia michuano ya Ndondo  Cup lakini akianza kwa kuzungumzia mchezo wao dhidi ya Kinondoni FC.

“Mechi ya leo ilikuwa ni nzuri, ngumu na yenye ushindani vijana wameonesha uwezo lakini timu yetu ilikuwa bora kuliko Kinondoni FC. Mpaka sasa tunapointi saba tukiwa tunaongoza kundi letu”.

“Ndondo Cup ni mashindano mazuri, kwanza yanaleta msisimko kwa vijana wanaotaka kucheza na kuonesha uwezo lakini kuna wachezaji wenye majina kubwa kwenye soka la Tanzania ambao wanatupa changamoto sisi vijana na haya mashindano yanaonekana yanatija”.

IMG_0347


Viewing all articles
Browse latest Browse all 565

Trending Articles



<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596347.js" async> </script>