Quantcast
Channel: NYINGINE – ShaffihDauda
Viewing all articles
Browse latest Browse all 565

KMC kufanyiwa party kusherekea ligi kuu

$
0
0

Baada ya kusubiri kwa takribani miaka miwili hatimaye timu ya manispaa ya kinondoni kmc leo imefanikiwa kupanda ligi kuu tanzania bara baada ya kupata ushindi wa goli 1-0 ugenini dhidi ya JKT Mlale kwenye uwanja wa majimaji, Songea.

Bao pekee la mchezo huo limefungwa na kiungo abdulhalim humoud dakika ya 45 kipindi cha kwanza lililodumu hadi dakika ya mwisho.

Kocha wa KMC Fred Felix Minziro ndiyo shujaa kwa upande wa timu hiyo ambaye pia aliisadia Singida United kupanda VPL msimu uliopita.

“Nawashuru viongozi wetu kwa kututia hamasa hususan katika mechi hizi tatu za mwisho ambazo tulijiwekea malengo ya kushinda zote ili tuweze kuingia ligi kuu, hamasa waliyotupa viongozi wetu ndiyo imefanya wachezaji wetu kujituma kwa nguvu sana.”

Tumezoea kumuona mwasyika akicheza kama mlinzi wa kushoto lakini katika mechi mbili za mwisho minziro amemtumia kama mshambuliaji.

“Eneo la ushambuliaji halikuwa vizuri sana hasa katika mechi kadhaa zilizopita walikuwa wakikosa magoli mengi kwa hiyo niliamua kumtumia mwasyika na ameleta tija ndani ya timu,” Minziro.

Mstahiki Mayor wa Manispaa ya Kinondoni Benjamini Sitta ameongozana na timu hadi mkoani Ruvuma lakini pia amekuwa karibu na timu kwa baadhi ya mechi za mwisho.

“Tumetumia nguvu kubwa sana kumpata kocha Minziro yote ilikuwa ni kuhakikisha kwamba mwaka huu timu inapanda kucheza ligi kuu. Kama mnavyojua mwaka jana timu hii iliongoza hadi dakika za mwisho haikufanikiwa, mwaka juzi vilevile kwa hiyo mwaka huu nikiwa Mayor nikaamua kwenda na wachezaji bega kwa bega,” Benjamini Sitta.


Viewing all articles
Browse latest Browse all 565

Latest Images

Trending Articles



Latest Images

<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596347.js" async> </script>