Quantcast
Channel: NYINGINE – ShaffihDauda
Viewing all articles
Browse latest Browse all 565

Azam imefanikiwa kupata ushindi wa pili bila ‘Wahispania’

$
0
0

dsc_0103

Azam FC imepata ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Zimamoto katika mchezo wa Kundi B michuano ya Mazpinduzi Cup inayoendelea visiwani Zanzibar.

dsc_0137

Goli pekee katika mchezo huo limefungwa na Shabani Idd dakika ya 76 kipindi cha pili baada ya kufanikiwa kumpita golikipa wa Zimamoto kisha kufunga bao hili kiulani.

dsc_0116

Mchezo kati ya Azam vs Zimamoto ulianza saa 10:00 ikiwa ni mchezo wa kwanza wa Kundi A wakati mchezo mwingine wa kundi hilo utaikutanisha Yanga dhidi ya Jamhuri kuanzia saa 2:15 usiku.

Ushindi wa leo ni wa pili kwa Azam FC bila makocha wao wakihispania ambao walitimuliwa juma lililopita. Ushindi wa kwanza kwa Azam bila makocha hao ulikuwa ni mchezo wa ligi kuu Tanzania bara dhidi ya Tanzania Prisons.

dsc_0127

Kwa sasa Azam ipo chini ya kocha wa timu ya vijana wa U-20 Idd Cheche ambaye anaisimamia kwa muda wakati mchakato wa kusaka kocha mkuu unaendelea.

dsc_0121


Viewing all articles
Browse latest Browse all 565

Trending Articles



<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596347.js" async> </script>